Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

General Assembly

Habari za UN- Mtazamo wa kimataifa; Habari za kiutu

Kunani?

Wavuti wa Radio ya Umoja wa Mataifa unafungwa rasmi mwishoni mwa mwezi Januari 2018. Nafasi yake itachukuliwa na ukurasa mpya ambao tuna imani utawapatia wasikilizaji na washirika katika vituo mbali mbali vya radio duniani, taarifa bora zaidi katika muundo tofauti.

Idara ya Habari kwa Umma ya Umoja wa Mataifa inayo furaha kuzindua wavuti huo ambamo kwao utapata taarifa katika mifumo yote. Mabadiliko haya kutoka Radio ya Umoja wa Mataifa hadi Habari za UN ni matokeo ya tafiti za kina kuhusu matumizi na mahitaji ya hadhira yetu.

Sudan Kusini ni hatari kwa watoa misaada-UNICEF

Hali ya sasa ya kiusalama nchini Sudan Kusini si shwari kwa wafanyakazi wanaotoa misaada.

Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF, Henrietta H. Fore amesema hayo leo akieleza kuwa shirika lake pamoja na mengine ya misaada nchini Sudan Kusini yanafanya kazi katika mazingira hatari wakati wakitoa misaada muhimu inayohitajika kwa watoto pamoja  na vijana.

Dunia ni lazima ishikamane na kuwa na ujasiri 2018:Guterres

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, ameyataka mataifa duniani kuwa na kile alichoita umoja na ujasiri katika vita vya dhidi ya mgogoro unaondelea pamoja alichokiita hatari mpya. Katibu Mkuu António Guterres ametoa wito huo wa busara mjini New York Marekani hii leo wakati akilihutubia baraza kuu la Umoja wa Mataifa, na kufafanua maeneo ambayo atayapa kipaumbele kwa mwaka huu wa 2018.

Katika ujumbe wake ametaja masuala 12 ya kuyatilia mkazo na kisha kusisitiza moja kubwa la kuwawezesha wanawake popote pale.

(SAUTI YA ANTONIO GUTERRES-KATIBU MKUU)

Sikufahamu Ureno zaidi ya mchezaji nyota Ronaldo- mhamiaji

Nchini Syria vita ikiingia mwaka wa saba, wananchi bado wanaendelea kukimbia nchi hiyo ili kusaka hifadhi ugenini. Takwimu za Umoja wa Mataifa zinaonyesha kwamba zaidi ya wasyria milioni 7 wamekimbilia ugenini na wanapatiwa hifadhi katika nchi ya tatu. Miongoni mwao ni Enas Fathallah na familia yake ambao sasa wanaishi Ureno, nchi ambayo awali hawakuijua kabisa zaidi ya kufahamu kuwa ndiko anakotoka mwanasoka maarufu duniani, Cristiano Ronaldo. Je yapi haliwasibu? Assumpta Massoi anaangazia kwenye makala hii.