Umoja wa Mataifa walaani shambulio hekaluni Jerusalem
Mratibu maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu mchakato wa amani mashariki ya kati Robert Serry ameeleza kuchukizwa na shamblio la asubuhi ya leo katika hekalu mashariki mwa Jerusalem.
Mratibu huyo maalum amesisitiza katika taarifa yake kuwa Umoja wa Mataifa unatoa wito wa dharura kwa pande zote kufanya kila liwezekanalo kuepusha kuendelea kwa hali liyopo ya mvutano Jerusalem.
Amesema anaomboleza pamoja na familia za wahanga wa shambulio hilo.