Mtu 1 huuawa kila saa kwa bomu au kilipuzi - UN
Mabomu, vilipuzi na vifaa vingine vya mlipuko vinaendelea kuua na kujeruhi watu katika maeneo mengi yenye changamoto kubwa za migogoro duniani na matokeo yake vifaa hivyo vya mlipuko, kwa wastani hukatili Maisha ya mtu mmoja kila saa, na waathirika wakubwa wakiwa ni watoto kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa.