Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Walinda amani wa UN kikosi cha 6 cha Tanzania nchini CAR wasaidia katika matibabu kwa wananchi.
©Kapteni Mwijage Francins Inyoma

TANBAT 6 wafanya usafi na kutoa msaada wa vifaa tiba CAR

Walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutokaTanzania wanaohudumu chini ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR, MINUSCA wametoa misaada mbalimbali kwa jamii wanazolinda kama moja ya sehemu ya kuimarisha utangamano na maelewano kati yao na jamii wanayoilinda. Tupate taarifa zaidi kutoka kwa Kapten Mwijage Inyoma. 

Sauti
1'56"
Csaba Kőrösi (kushoto) Rais wa mkutano wa 77 wa Baraza Kuu la UN akikabishi rungu la kuongoza mkutano kwa Rais wa mkutano wa 78 wa Baraza Kuu la UN (UNGA78). Kulia kabisa ni Naibu Katibu Mkuu wa UN Amina J. Mohammed
UN /Manuel Elias

UNGA 77 yafunga pazia, Rais wa UNGA78 ala kiapo

Mkutano wa 77 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa umekunja jamvi asubuhi ya tarehe 5 Septemba 2023, jijini New York, Marekani kwa Rais wa mkutano huo anayemaliza muda wake Csaba Kőrösi akisisitiza kuwa licha ya mikingamo ya kijiografia, ushirikiano baina ya nchi haukwepeki.

Torrez Omoll, muasisi wa Mngaro Mtaani, shirika la kujitolea kusaidia watu maskini na wagonjwa nchini Kenya.
UN News/Thelma Mwadzaya

Mng’aro Mtaani Kenya: Ukimtendea mtu wema, naye atamtendea mwingine - Torrez Omoll

Leo ni siku ya kimataifa ya hisani au kuwaonea huruma wagonjwa na maskini, siku iliyopitishwa na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kutambua mchango wa Hayati Mama Teresa wa Calcuta nchini India ambaye pia ni mshindi wa Tuzo ya amani ya Nobel. Hayati Mama Teresa alianzisha shirika la watawa wa huruma likiendesha makazi ya kuhudumia maskini na wagonjwa.  

Benge Mukengere, Kiongozi wa shirika la AFNAC linalohudumia watoto na wanawake wazee katika mji wa Beni, jimboni Kivu Kaskazini mashariki mwa DRC.
UN News/George Musubao

Moyo wa fadhila wa Mama Teresa bado unazingatiwa huko Beni, DRC

Katika maadhimisho ya siku ya kimataifa ya hisani au fadhila tunamulika vituo au watu wanaojitolea kusaidia maskini na wagonjwa ikiwa ni katika kutambua siku hii iliyopitishwa na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kutambua mchango wa Hayati Mama Teresa wa Calcuta nchini India ambaye pia ni mshindi wa Tuzo ya amani ya Nobel. Hayati Mama Teresa alianzisha shirika la watawa wa huruma likiendesha makazi ya kuhudumia maskini na wagonjwa. 

Mwanaharakati Valdecir Nascimento katika kikao cha Pili cha Jukwaa la Kudumu la Watu Wenye Asili ya Afrika
UN News/ Pauline Batista

Watu wa asili ya Afrika kutoshirikishwa kwa uthabiti katika masuala ya umma kunazuia maendeleo ya haki na usawa wa rangi - ripoti ya UN

Watu wenye asili ya Afrika wanaendelea kukabiliwa na changamoto kubwa za ushiriki wa maana katika masuala ya umma katika nchi nyingi kutokana na ubaguzi wa kimfumo, kutengwa na mara nyingi kunakotokana na urithi wa utumwa na ukoloni, kulingana na ripoti iliyotolewa leo na Ofisi ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa mjini Geneva, Uswisi.