Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Upotevu na utupaji wa chakula unahitaji kupunguzwa ili kulisha kwa ufanisi zaidi idadi ya watu inayoongezeka ulimwenguni.
© FAO/Heba Khamis

Kwa nini kuzuia upotevu na utupaji wa chakula ni muhimu na jukumu la kila mtu: FAO

Katika siku ya kimataifa ya uhamasishaji kuhusu uelewa wa Upotevu na utupaji wa chakula, shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo FAO linataka kila mtu atambue ni kwanini kuzuia na kupumguza upotevu na utupaji wa chakula ni muhimu hasa katika kuchangia mabadiliko ya mifumo ya chakula na utimizaji wa malengo ya maendeleo endelevu SDGs.

Sauti
2'30"
Rais wa Baraza Kuu la UN Balozi Dennis Francis akiwapatia waandishi wa habari tathmini ya vikao vya ngazi ya juu vya mkutano wa 78 wa Baraza Kuu la UN (UNGA78).
UN /Eskinder Debebe

SDGs zilikuwa 'mdomoni' mwa kila mtoa hotuba – Rais UNGA78

Kile nilichoshuhudia ni jamii ya kimataifa iliyojizatiti upya kukamilisha utekelezaji wa malengo ya maendeleo endelevu, SDGs ifikapo mwaka 2030, amesema Rais wa Mkutano wa 78 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA78, Dennis Francis akizungumza na waandishi wa habari, ikiwa ni mara ya kwanza tangu ashike wadhifa huo.

Watu waliohama makazi yao wakiwa katika uwanja wa ndondi katikati mwa jiji la Port-au-Prince baada ya kukimbia nyumba zao wakati wa mashambulizi ya magenge mnamo Agosti 2023.
© UNOCHA/Giles Clarke

Hali si hali Haiti, tuwasaidie polisi wa kitaifa - Türk

Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Kibinadamu, Volker Türk, hii leo ametoa wito kwa jumuiya za kimataifa kusaidia ujumbe wa usalama kuwasaidia Polisi wa Kitaifa wa Haiti (HNP) kupambana na vurugu zinazoendelea katika ngazi zote za jamii na kuzidisha hali mbaya ya usalama na ubinadamu pamoja na mgogoro wa haki.