Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Mwambata wa jeshi Brigedia Generali Absolomon Lyanga Shausi akisalimiana na Afisa wa Polisi wa NEPAL iliyopo chini ya MINUSCA mara baada ya kumaliza ziara yake ya kujitambulisha kwa walinda amani wa Umoja wa Mataifa wanahudumu chini ya MINUSCA nchini CAR.
TANBAT 6

Mwambata jeshi wa Tanzania nchini CAR asifu utimamu wa wanajeshi wa Tanzania

Mwambata jeshi wa Tanzania anayehudumu kazi yake Jamhuri ya Afrika ya kati Brigedia Jenerali Absolomon Lyanga Shausi amefanya ziara ya kutembelea kikosi cha walinda amani wa Tanzania TANBAT6 wanaohudumu chini ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati MINUSCA ili kujitambilisha tangu kikosi hicho kianze shughuli ya ulinzi wa amani kikipokea majukumu kutoka kwa kikosi cha TANBAT5 mwishoni mwa mwaka jana.

Sauti
2'31"
Gibson Kawago (katikati) akibadilishana mawazo na vijana wenzake wakati ya Jukwaa la Vijana kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa. Aprili 2023, New York, USA.
UN

Nimekuja UN kuuonesha ulimwengu ni vitu gani vijana Tanzania tunafanya – Gibson Kawago

Jukwaa la Vijana la Baraza la Umoja wa Mataifa la Kiuchumi na Kijamii (ECOSOC) la mwaka 2023 limeng’oa nanga jana tarehe 26 April ambapo maelfu ya viongozi vijana kutoka duniani kote wanakusanyika katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York kujadili pamoja na mambo mengine, masuala yanayolenga kuharakisha kujikwamua kutoka janga la COVID-19 na utekelezaji kamili wa Ajenda ya 2030 ya Malengo ya Maendeleo Endelevu.

Susan Auma Mang'eni Katibu Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Biashara Ndogo ndani ya wizara mpya ya ushirika na ujasiriamali nchini Kenya, akizungumza katika Kongamano la Uchumi Duniani jijini New York.
UN News/Anold Kayanda

Kenya rasilimali watu tunayo tunachohitaji ni ufadhili kuiendeleza ili kutimiza malengo: Susan Auma

Jukwaa la Umoja wa Mataifa la ufadhili kwa ajili ya maendeleo 2023 FfD linaendelea kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa katika jaribio la kubadilisha mfumo wa fedha wa kimataifa na kurejesha ajenda ya maendeleo endelevu ya 2030 katika mstari unaotakiwa ikiwa imesalia chini ya miaka saba kufikia ukomo.

Sauti
3'11"
Jamii la kabila la watu wa asili ambao wanaishi kwenye misitu iliyo ndani zaidi katika ukingo wa Mto Congo nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC.
UNICEF/Vincent Tremeau

Miti ya migunga yarejesha matumaini kwa wakazi wa msitu wa Congo

Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, mradi unaofadhiliwa na Benki ya Dunia wa kupanda miti aina ya migunga imeondoa tishio la ukataji miti holela kwenye msitu wa bonde la mto Congo, ambao ni wa pili kwa ukubwa duniani katika kufyonza hewa ya ukaa na sasa wananchi wananufaika sio tu kwa kupata mkaa bali pia hata watu wa jamii ya asili wanaweza kupata kitoweo porini.

Sauti
2'16"
Immaculée Songa, manusura wa mauaji ya kimbari ya mwaka 1994 dhidi ya watutsi nchini Rwanda akiwa mbele ya maonesho yanayofanyika Umoja wa Mataifa. Gauni hilo ni la mtoto wake aliyeuawa wakati wa mauaji.
ONU Info/Florence Westergard

Ujumbe wangu kwa wanangu, “Katu sitowasahau,” : Manusura mauaji ya Rwanda

Immaculée Songa Mukantaganira, manusura wa mauaji ya kimbari nchini Rwanda akihojiwa na Idhaa ya Umoja wa Mataifa kuelekea kumbukizi ya miaka 29 tangu mauaji ya kimbari nchini Rwanda anasema, “nguo hizo zinanipatia taswira ya mwisho ya binti zangu, jinsi maisha yao yalivyofupishwa, jinsi walikuwa watoto na malaika.”

Sauti
4'39"
Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO nchini Tanzania limeendesha warsha ya siku 2 kwenye mkoa wa Kigoma ulioko magharibi mwa taifa hilo kuwapatia wadau matokeo ya utafiti wa jinsi ya kuimarisha usawa wa kijinsia kwenye sekta ya uvuvi.
Idhaa ya UN

FAO Tanzania yachukua hatua kukwamua wavuvi wanawake na wanaume kupitia FISH4ACP

Nchini Tanzania, shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO kupitia  mradi  wake  FISH4ACP  limepokea matokeo ya Utafiti kuhusu Usawa wa Kinjisia katika Masuala ya Uvuvi, moja ya hoja ambayo ikitekelezwa vema itasaidia kufanikisha malengo ya maendeleo endelevu, SDGs hasa la kutokomeza njaa na kuondokana na umaskini.

Sauti
2'26"