Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Rais wa UNGA76 Abdullah Shahid akifunga mjadala mkuu wa UNGA76 jijini New York, Marekani 27 Septemba 2021
UN/Cia Pak

Rais wa UNGA76 afunga pazia la mjadala mkuu; asema ushirikiano wa kimataifa ungali hai

Hatimaye mjadala mkuu wa mkutano wa 76 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA76 umefunga pazia leo Jumatatu katika makao makuu ya Umoja huo jijini New York, Marekani huku Rais wa Baraza hilo Abdullah Shahid akisema mkutano huo umefanyika kwa mafaniko makubwa katikati ya janga la Corona au COVID-19 huku akitaja sababu za mafanikio hayo kuwa ni hatua bora za kupunguza maambukizi na viwango vya juu vya chanjo.