Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Utoaji wa chanjo dhidi ya COVID-19 nchini Kenya.
WHO Video

Kenya yaanza kutoa chanjo dhidi ya COVID-19 

Serikali ya Kenya inaendelea na kampeni ya chanjo dhidi ya corona au COVID-19 baada ya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF kupata na kusafirisha dozi zaidi ya milioni moja hadi Nairobi kupitia mkakati wa kimataifa wa upatikanaji wa chanjo COVAX. 

 

Sauti
2'43"
Katibu Mkuu Antonio Guterres akihudhuria kuoneshwa wazi kwa 'Darasa la Janga' katika Makao Makuu ya UN ili kuangazia hitaji la serikali kuweka kipaumbele kufungua shule.
UN Photo/Eskinder Debebe)

Watoto milioni 168 wamepoteza mwaka 1 wa masomo, hilo nalo ni janga - Guterres 

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres hiI leo Machi 2 ametembelea eneo katika moja ya viwanja vya Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York Marekani, ambalo limetumiwa na shirika la kuhudumia watoto la Umoja wa Mataifa UNICEF, kutoa wito kuhusu dharura ya elimu iliyotokana na COVID-19 na kukuza ufahamu kuhusu uhitaji wa serikali kuzifungua shule.