Ushirikiano wa kimataifa ni muhimu zaidi sasa kukabili dharura ya tabianchi- Guterres
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa leo limekuwa na mjadala kuhusu vitisho vya amani na usalama duniani visababishwavyo na janga la tabianchi ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema janga la tabianchi ni changamoto ya ushirikiano wa kimataifa katika zama za sasa.