Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Uwekezaji wa nje umeongezeka:UNCTAD

Taarifa iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la biashara, uchumi na maendeleo UNCTAD inaonyesha kwamba uwekezaji wa moja kwa moja wa nje umeongezeka kwa asilimia 13 kwa mwaka 2010 ingawa uko chini kidogo ya ule wa 2007 kabla ya mdororo wa uchumi.

Uwekezaji katika elimu umeongezeka Afrika:UNESCO

Ripoti iliyochapishwa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la elimu, sayansi na utamaduni UNESCO inasema nchi za Afrika Kusini mwa jangwa la Sahara zimeongeza uwekezaji na matumuzi ya masuala ya elimu kwa zaidi ya asilimia 6 kila mwaka katika muongo uliopita.

Pillay akaribisha ripoti ya uchunguzi Sri Lanka

Mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa Navi Pillay amekaribisha kutolewa kwa ripoti iliyoangazia machafuko ya Sri Lanka na ameunga mkono mwito uliotolewa na ripoti hiyo ambayo imetaka kufanyika kwa uchunguzi zaidi wa kimataifa.