Hapa na pale
Ijumatano, KM Mdogo na Mshauri wa UM juu ya Misaada ya Daharura, John Holmes alikamilisha ziara ya siku tatu Ethiopia. Ijumanne, Holmes alizuru eneo la wenyeji wa asli ya Kisomali, sehemu ya nchi iliodhurika sana na ukame, pamoja na bei kubwa ya chakula na mgogoro unaozidi kuendelea katika eneo lao. Kwenye kituo cha ukaguzi juu ya hadhi za wahamiaji, Holmes akikutana na wenyeji raia wa Kisomali na Kiethiopia waliokata tama ya maisha na ambao walitaka kusaidiwa kihali, halan. Alikumbusha Holmes ya kuwa ukosefu wa misaada ya kiutu umewalazimisha wahamiaji wingi wa Kiethiopia kutafuta hifadhi ya kisiasa, kwa matumaini ya kupatiwa chakula, makazi na huduma za afya.