Ubashiri wa hali ya hewa ni muhimu kupunguza umasikini na kutunza rasilimali ya maji
Michel Jarraud, Mkurugenzi wa Shirika la UM juu ya Upimaji wa Hali ya Hewa Duniani (WMO) aliwaambia wawakilishi waliohudhuria Mkutano wa Dunia juu ya Maji unaofanyika kwenye mji wa Montpellier, Ufaransa kwamba ni muhimu kwa nchi wanachama kutumia ujuzi wa kisasa wa kutabiri hali ya hewa wakati wanapoandaa miradi ya maendeleo ya uchumi na kupunguza umaskini unaochochewa na athari kubwa za mabadiliko ya hali ya hewa, hususan wanapotathminia akiba ya maji.