Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Mpatanishi wa UA kwa Darfur ana matumaini ya kutia moyo juu ya amani

Wajumbe wa UM na UA wanaoshughulikia suala la Darfur, yaani Jan Eliasson na Salim Ahmed Salim, karibuni walikamilisha duru nyengine ya zile juhudi za kufufua tena mazungumzo ya jumla kuhusu amani katika Darfur, baina ya Serikali ya Sudan na makundi ya waasi. Jumbe Omari Jumbe, Ofisa wa Habari wa Shirika la Ulinzi wa Amani la UM Sudan (UNMIS) alipata fursa ya kumhoji Mpatanishi wa Umoja wa Afrika Salim hivi majuzi alipozuru mji wa Juba, Sudan kusini.

'Tuufanye 2008 kuwa mwaka wa kufyeka hali duni kwa mafukara bilioni' - Ban Ki-moon

KM wa UM Ban Ki-moon aliitisha kikao maalumu mwanzo wa 2008, kuzungumza na wanahabari wa kimataifa waliopo Makao Makuu mjini New York, ambapo alitathminia hali halisi juu ya kazi za UM. Kadhalika, alichukua fursa hiyo kutufafanulia mwelekeo anaopendelea uzingatiwe na jumuiya ya kimataifa katika kuimarisha kazi za UM, pamoja na kudhibiti bora miradi inayotekelezwa na mashirika yake kadha wa kadha katika sehemu mbalimbali za dunia. ~

'Tuufanye 2008 kuwa mwaka wa kufyeka hali duni kwa mafukara bilioni' - Ban Ki-moon

KM wa UM Ban Ki-moon aliitisha kikao maalumu mwanzo wa 2008, kuzungumza na wanahabari wa kimataifa waliopo Makao Makuu mjini New York, ambapo alitathminia hali halisi juu ya kazi za UM. Kadhalika, alichukua fursa hiyo kutufafanulia mwelekeo anaopendelea uzingatiwe na jumuiya ya kimataifa katika kuimarisha kazi za UM, pamoja na kudhibiti bora miradi inayotekelezwa na mashirika yake kadha wa kadha katika sehemu mbalimbali za dunia. ~

Wapatanishi wa UM/UA watangaza matumaini mema kurudisha amani Darfur

Wajumbe Maalumu wa Kimataifa kwa Darfur, yaani Jan Eliasson akiwakilisha Umoja wa Mataifa (UM), pamoja na Salim Ahmed Salim anayewakilisha Umoja wa Afrika (UA), baada ya kuzuru Sudan kwa wiki moja, ambapo walikutana kwa mashauriano na wawakilishi wa Serikali pamoja na wajumbe wa makundi ya waasi, waliripoti kuwa na matumaini ya kutia moyo kwamba wataweza kufufua tena karibuni yale mazungumzo ya Sirte ya kukomesha mzozo wa jimbo la vurugu la Sudan magharibi.

Wapatanishi wa UM/UA watangaza matumaini mema kurudisha amani Darfur

Wajumbe Maalumu wa Kimataifa kwa Darfur, yaani Jan Eliasson akiwakilisha Umoja wa Mataifa (UM), pamoja na Salim Ahmed Salim anayewakilisha Umoja wa Afrika (UA), baada ya kuzuru Sudan kwa wiki moja, ambapo walikutana kwa mashauriano na wawakilishi wa Serikali pamoja na wajumbe wa makundi ya waasi, waliripoti kuwa na matumaini ya kutia moyo kwamba wataweza kufufua tena karibuni yale mazungumzo ya Sirte ya kukomesha mzozo wa jimbo la vurugu la Sudan magharibi.

Wapatanishi wa UM/UA watangaza matumaini mema kurudisha amani Darfur

Wajumbe Maalumu wa Kimataifa kwa Darfur, yaani Jan Eliasson akiwakilisha Umoja wa Mataifa (UM), pamoja na Salim Ahmed Salim anayewakilisha Umoja wa Afrika (UA), baada ya kuzuru Sudan kwa wiki moja, ambapo walikutana kwa mashauriano na wawakilishi wa Serikali pamoja na wajumbe wa makundi ya waasi, waliripoti kuwa na matumaini ya kutia moyo kwamba wataweza kufufua tena karibuni yale mazungumzo ya Sirte ya kukomesha mzozo wa jimbo la vurugu la Sudan magharibi.

UM kuomba dola milioni 42 kuhudumia misaada ya kiutu kwa Wakenya 500,000

John Holmes, Mshauri wa UM juu ya Misaada ya Dharura karibuni aliitisha mkutano maalumu na waandishi habari kwenye Makao Makuu mjini New York, na alidhihirisha kwamba machafuko yaliojiri Kenya baada ya matokeo ya uchaguzi kutangazwa yaliathiri kihali watu 500,000. Kwa hivyo UM unahitajia kufadhiliwa na wahisani wa kimataifa msaada wa dharura, uliokadiriwa dola milioni 42 kuhudumia misaada ya kiutu na faraja ya kimaisha umma huu ulioathirika na vurugu liliofumka Kenya mwanzo wa mwaka.

UM kuomba dola milioni 42 kuhudumia misaada ya kiutu kwa Wakenya 500,000

John Holmes, Mshauri wa UM juu ya Misaada ya Dharura karibuni aliitisha mkutano maalumu na waandishi habari kwenye Makao Makuu mjini New York, na alidhihirisha kwamba machafuko yaliojiri Kenya baada ya matokeo ya uchaguzi kutangazwa yaliathiri kihali watu 500,000. Kwa hivyo UM unahitajia kufadhiliwa na wahisani wa kimataifa msaada wa dharura, uliokadiriwa dola milioni 42 kuhudumia misaada ya kiutu na faraja ya kimaisha umma huu ulioathirika na vurugu liliofumka Kenya mwanzo wa mwaka.

UM kuomba dola milioni 42 kuhudumia misaada ya kiutu kwa Wakenya 500,000

John Holmes, Mshauri wa UM juu ya Misaada ya Dharura karibuni aliitisha mkutano maalumu na waandishi habari kwenye Makao Makuu mjini New York, na alidhihirisha kwamba machafuko yaliojiri Kenya baada ya matokeo ya uchaguzi kutangazwa yaliathiri kihali watu 500,000. Kwa hivyo UM unahitajia kufadhiliwa na wahisani wa kimataifa msaada wa dharura, uliokadiriwa dola milioni 42 kuhudumia misaada ya kiutu na faraja ya kimaisha umma huu ulioathirika na vurugu liliofumka Kenya mwanzo wa mwaka.

Ofisa wa Habari wa UNMIS asailia mpango wa amani kwa Darfur

Jumbe Omari Jumbe, Ofisa wa Habari wa Shirika la UM juu ya Ulinzi wa Aamani Sudan (UNMIS) anatuchambulia fafanuzi zake kuhusu juhudi za wapatanishi wa kimataifa juu ya Darfur, yaani Jan Eliasson wa Umoja wa Mataifa na Salim Ahmed Salim akiwakilisha Umoja wa Afrika. Wapatanishi Eliasson na Salim walikuwepo Sudan wiki hii kujaribu kufufua tena mazungumzo ya kusuluhisha mzozo wa Darfur kwa ridhaa ya makundi yote husika.~~Sikiliza idhaa ya mtandao kwa mahojiano kamili na Jumbe.