Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UM kuomba dola milioni 42 kuhudumia misaada ya kiutu kwa Wakenya 500,000

UM kuomba dola milioni 42 kuhudumia misaada ya kiutu kwa Wakenya 500,000

John Holmes, Mshauri wa UM juu ya Misaada ya Dharura karibuni aliitisha mkutano maalumu na waandishi habari kwenye Makao Makuu mjini New York, na alidhihirisha kwamba machafuko yaliojiri Kenya baada ya matokeo ya uchaguzi kutangazwa yaliathiri kihali watu 500,000. Kwa hivyo UM unahitajia kufadhiliwa na wahisani wa kimataifa msaada wa dharura, uliokadiriwa dola milioni 42 kuhudumia misaada ya kiutu na faraja ya kimaisha umma huu ulioathirika na vurugu liliofumka Kenya mwanzo wa mwaka.

Sikiliza taarifa kamili kwenye idhaa ya mtandao.