Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

'Tuufanye 2008 kuwa mwaka wa kufyeka hali duni kwa mafukara bilioni' - Ban Ki-moon

'Tuufanye 2008 kuwa mwaka wa kufyeka hali duni kwa mafukara bilioni' - Ban Ki-moon

KM wa UM Ban Ki-moon aliitisha kikao maalumu mwanzo wa 2008, kuzungumza na wanahabari wa kimataifa waliopo Makao Makuu mjini New York, ambapo alitathminia hali halisi juu ya kazi za UM. Kadhalika, alichukua fursa hiyo kutufafanulia mwelekeo anaopendelea uzingatiwe na jumuiya ya kimataifa katika kuimarisha kazi za UM, pamoja na kudhibiti bora miradi inayotekelezwa na mashirika yake kadha wa kadha katika sehemu mbalimbali za dunia. ~