Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari Mpya

Watu milioni 33 nchini Pakistani waliathiriwa na mafuriko makubwa yaliyokumba taifa hilo mwezi Septemba mwaka 2022
© WFP

Takribani watoto milioni 4 nchini Pakistani bado wanaishi kwenye maji machafu yaliyotwama- UNICEF

Nchini Pakistani, janga la uhai wa mtoto bado ni changamoto kubwa kwenye maeneo yaliyokumbwa na mafuriko zaidi ya miezi minne iliyopita huku idadi ya maambukizi  ya magonjwa ya hewa na utapiamlo uliokithiri au unyafuzi ikiendelea kuongezeka, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto,  UNICEF wakati huu ambapo jumuiya ya kimataifa inajiandaa kwa ajili ya mkutano wa kuchangia taifa hilo la Asia ili lijenge mnepo dhidi ya majanga.

Sauti
2'29"
Walinda amani wa UN kutoka Tanzania waanzisha kampeni kutumia afya kuleta amani DRC
Picha: MONUSCO

Walinda amani wa UN kutoka Tanzania waanzisha kampeni kutumia afya kuleta amani DRC

Kikosi cha tisa cha ulinzi wa amani kutoka Tanzania, TANZBATT 9 kinachohudumu ndani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC Ujumbe wa Umoja wa Mataifa kulinda amani nchini DRC, MONUSCO, kimeanzisha kampeni iliyopewa jina la “Afya na Amani” ambayo inahusisha utoaji wa dawa za binadamu katika vituo vya Afya, Zahanati na Hospitali za baadhi ya maeneo ya uwajibikaji ya Kikosi hicho ndani ya mji wa Beni, kaskazini mashariki mwa DRC.

Sauti
5'37"
Mtoto wa miaka 14 mkimbizi kutoka Niher akiwa ameweka mkono wake katika geti akiwa kizuizini nchini Libya
© UNICEF/Alessio Romenzi

Waachilieni huru waliofungwa kwa kusimamia haki zao- Türk

Kufuatia kuanza kwa maadhimisho ya miaka 75 tangu kupitishwa kwa Tamko la Umoja wa Mataifa kuhusu haki za binadamu, UDHR, Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu haki za binadamu, Volker Türk ametoa wito kwa serikali duniani kote na mamlaka zote zinazoshikilia watuhumiwa kuwapatia msamaha au kuwaachilia huru wale wote walioswekwa ndani kwa kutekeleza haki zao za msingi.

Sauti
1'55"