Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari Mpya

Waudumu wa WHO wakiwa kwenye shughuli katika kambi ya kanyaruchinya wilayani Nyiragongo-Goma
UN News/ Byobe Malenga.

Chanjo dhidi ya Kipindupindu yaendelea Kivu Kaskazini, DRC- WHO

Kampeni ya utoaji wa chanjo dhidi ya ugonjwa wa kipindupindu  iliyoanza tarehe 25 mwezi huu huko Kivu Kaskazini nchini jamhuri ya Kidemokraia ya Congo, DRC imekunja jamvi jana Jumanne ya tarehe 30 mwezi hu uwa Januari ambapo shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni WHO lilizindua kampeni hiyo ya chanjo kwa wakimbizi wa ndani katika kambi ya wakimbizi hao ya Kanyaruchinya wilayani nyiragongo katika mji wa Goma jimboni Kivu Kaskazini.

Sauti
5'30"
Jamii ya Benet nchini Uganda ambao bado hawana Utaifa.
UNHCR Video

Jamii ya Benet nchini Uganda yaiomba serikali kumaliza changamoto yao ya kutokuwa na utaifa: UNHCR

Baada ya zaidi ya takriban miongo minane ya kutokuwa na utaifa, jamii ya watu wa asili ya Benet nchini Uganda inahaha kuishi, na kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR bila kuwa na nyaraka rasmi muhimu haiwezi kupata huduma za msingi kama elimu na afya , na sasa jamii hiyo inaiomba serikali ya Uganda kumaliza zahma hiyo iliyowaghubika kwa miongo.

Sauti
3'6"
Wayahudi kutoka Subcarpathian Rus wanakabiliwa na mchakato wa uteuzi kwenye ramp huko Auschwitz-Birkenau, Poland.
US Holocaust Memorial Museum/Yad Vashem

Mauaji ya maangamizi makubwa yalikuwa kilele cha miongo ya chuki dhidi ya wayahudi: Guterres

Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya kumbukizi ya waathitrika wa mauaji ya maangamizi makubwa au Holocaust Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António  Guterres amesema mauaji hayo yalikuwa ni malimbikizo ya miongo ya chuki dhidi ya wayahudi ndio maana sasa ni wakati wa kuhakikisha chuki za aina yoyote ile zinakomeshwa duniani.

Sauti
2'23"
Walinda amani wa Umoja wa Mataifa, Kikosi cha 9 kutoka Tanzania, TANZBATT 9 katika doria ya barabara ya Mbau-Kamango
TANZBATT 9

Walinda amani wa UN kutoka Tanzania wafanya doria barabara inayounganisha DRC na Uganda

Kufuatia mashambulizi yanayofanywa na makundi mbalimbali ya waasi kwa raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC hususani mashariki mwa nchi hiyo ya pili kwa ukubwa wa eneo barani Afrika, walinda amani wa Umoja wa Mataifa wa kikosi cha 9 kutoka Tanzania, TANZBATT 9 kinachohudumu katika kikosi cha Umoja wa Mataifa cha kujibu mashambulizi cha FIB-MONUSCO, wamefanya doria katika barabara ya Mbau-Kamango nje ya mji wa Beni jimboni Kivu Kaskazini. 

Sauti
1'45"