Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari Mpya

 Uunganisho wa kidijitali, katika maeneo kama India, ni muhimu sana kuondokana na janga hili, na kwa urejeshaji endelevu na unaojumuisha.
United Nations/Chetan Soni

 Mkutano wa dunia wa mawasiliano waanza nchini Rwanda 

Mkutano wa kimataifa wa maendeleo ya mawasiliano umeanza leo mjini Kigali nchini Rwanda ukiwa na lengo la kupitisha mwongozo wa kimataifa wa mabadiliko ya kidigitali ili hatimaye kusaidia kuweka ufikiaji wa maana wa teknolojia za kidijitali mikononi mwa mabilioni ya watu duniani kote na kuhakikisha wananchi wasiounganishwa na mtandao wanaunganisha ili kufikia malengo ya maendeleo endelevu SDGs.

Sauti
1'27"
Samaki wakiogelea katika Bahari ya Sham
© Ocean Image Bank/Brook Peters

Bahari ni uhai, sio kwangu mimi tu bali kwa Wakenya wote: Bernadatte Loloju 

Katika kuelekea siku ya bahari duniani ambayo kila mwaka huadhimishwa Juni 8 tutakuletea sauti za watu mbalimbali wakizungumzia kwa nini bahari ni muhimu kwao. Maudhui ya mwaka huu ya siku ya bahari ni “kuhuisha hatua ya pamoja kwa ajili ya bahari” ikichagiza serikali, mashirika, asasi za kiraia na wadau wote kuchukua hatua ili kuilinda bahari na rasilimali zake kwa faida ya kizazi cha sasa na vijavyo .

Sauti
1'30"
UNICEF nchini Rwanda kwa kushirikiana na Bodi ya Madini nchini humo wamefanikiwa kuanzisha vituo viwili vya kulea watoto wadogo wenye umri kati ya miaka 0 mpaka 6 kwa ajili ya kusaidia wazazi wanaofanya kazi migodini.
UNICEF/2022/Mucyo

UNICEF Rwanda yawezesha uanzishwaji wa vituo vya kulelea watoto wa wafanyakazi wa migodi

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF nchini Rwanda kwa kushirikiana na Bodi ya Madini nchini humo wamefanikiwa kuanzisha vituo viwili vya kulea watoto wadogo wenye umri kati ya miaka 0 mpaka 6 kwa ajili ya kusaidia wazazi wanaofanya kazi migodini waweze kuwa na uhakika wa sehemu wanapowaacha watoto pindi waendapo kujitafutia kipato.

Sauti
3'10"