Zaidi ya asilimia 50 ya hewa ya Oksijeni yatoka baharini lakini bado tunaichafua- Guterres
Ongezeko la kiwango cha maji ya bahari, kwa joto la maji ya bahari, kiwango cha asidi baharini na kiwango cha juu cha hewa ya ukaa baharini, vinatishia ustawi wa bahari ambayo ni tegemeo la binadamu, amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres katika ujumbe wake hii leo ambayo ni siku ya bahari duniani.