Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari Mpya

Sidonie, mwenye umri wa miaka 10, akiwa mbele ya darasa la shule yake ya msingi Kitambo iliyoko mji mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, Kinshasa.
© UNICEF/Josue Mulala

Elimu ya sasa inapitia janga kubwa: Tuirekebishe kwa mustakabali wa watoto

Ingawa msemo wa haki ya binadamu umezoelekea, hakuna haki ya binadamu yoyote ambayo imetolewa bure bila kupiganiwa, vivyo hivyo inapaswa kuwa kwa elimu, amesema Leonardo Garnier, Mshauri Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mkutano wa Ngazi ya juu wa Umoja wa Mataifa kuhusu marekebisho ya mfumo wa elimu duniani, mkutano unaoanza Ijumaa hii kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa. Kufahamu msingi wa kauli hiyo, 

Sauti
2'
Tarehe 16 mwezi Juni mwaka 2022 mtoto wa kike akitumia pampu ya mkono kupata maji kutoka bwawa la mchanga lililojengwa na UNICEF huko Kanyangapus kaunti ya Tukrana nchini Kenya.
© UNICEF/Paul Kidero

Mabwawa ya mchanga Turkana yaepusha wanawake kutembea kilometa 10 kusaka maji

Katika Kijiji cha Kanyangapus Kaunti ya Turkana nchini Kenya hali ya ukame ni mbaya sana kila kona na moja ya athari kubwa zilizoambatana nao ni ukosefu wa maji.  Mabwawa ya mchanga yamekuwa suluhu bunifu inayozisaidia kaunti nyingi zilizo katika hali ya nusu jangwa nchini Kenya na shukrani kwa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF kwa kufadhili wa mradi huo wa ujenzi wa mabwawa ya mchanga na pampu za maji, sasa adha ya maji katika kaunti ya Turkana imepungua na hususan kwa wanawake wanaolazimika kwenda umbali mrefu kusaka maji. 

Sauti
2'40"
Vurugu za magenge mjni Port-au-Prince, Haiti, zinawatia hofu watu wazima na watoto vile vile.
UNDP Haiti/Borja Lopetegui Gonzalez

Licha ya vikwazo, WFP yaendelea kuokoa maisha Haiti 

Nchini Haiti, ambako karibu nusu ya idadi ya watu tayari hawana uhakika wa chakula, njaa inatazamiwa kuongezeka huku kukiwa na ongezeko la mfumuko wa bei, gharama kubwa za chakula na mafuta na kuzorota kwa usalama, linaonya Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani, WFP ingawa linaendelea kutoa msaada kwa Wahaiti walio katika mazingira hatarishi.

Sauti
2'30"
Watoto wa Darfur Kaskazini kambi ya wakimbizi wa ndani ya Abo Shouk ambako UNAMID imekarabati darasa.
UN Photo/Albert Gonzalez Farran

Vita, Machafuko na majanga mengine vyatawanya watoto milioni 36.5 mwaka 2021: UNICEF 

Vita, machafuko na mjanga mengine vimewaacha watoto milioni 36.5 wakitawanywa kutoka majumbani kwao hadi kufikia mwisho wa mwaka 2021 kwa mujibu wa takwimu mpya zilizotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF ambalo linasema idadi hiyo ni kubwa kabisa kurekodiwa tangu vita ya pili ya dunia.

Sauti
3'36"
Brigedia Jenerali George M. Itang'are, Mwambata wa Kijeshi Ubalozi wa Kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa (katikati) akiwa ameshikilia moja ya nishani ya Dag Hammarskjöld ambayo walitunukiwa walinda amani wawili wa Tanzania w
Ofisi ya Mwakilishi wa kudumu wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kwenye Umoja wa Mataifa, New York, Marekani.

Mashujaa watanzania wawili miongoni mwa waliotunukiwa medali ya Dag Hammarskjold

Kuelekea siku ya kimataifa ya walinda amani ambayo itaadhimishwa Jumapili hii tarehe 29 Mei, Umoja wa Mataifa umetoa medali kuwatambua na kuwaenzi walinda amani majasiri. Miongoni mwa medali zilizotolewa ni ya Dag Hammarskjoldna kati ya waliotunukiwa ni askari wawili wa Tanzania waliouawa mwaka 2021 wakiwa katika majukumu ya ulinzi wa amani nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC.

Sauti
2'27"
Picha ya Picasso ya Guernica ikitundikwa upya nje ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa baada ya kusafishwa na wahifadhi.
UN Photo/Mark Garten)

Mchoro wa kihistoria wa Picasso unaofahamika kama Guernica warejeshwa UN

Mchoro wa kihistoria unaofahamika kama Guernica uliofumwa vizuri kwa nyuzi katika kitambaa kikubwa ukilenga kupinga vita na matukio yake, umerejeshwa tena katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa baada ya kuondolewa takribani mwaka mmoja uliopita ili usafishwe kitaalamu chini ya familia ya mfanyabiashara na mwanasiasa wa zamani wa Marekani, Marehemu Nelson Rockeffeler.

Sauti
2'30"
Katika umri wa miaka 22 tu, Mariama Camara Cire (katikati) ni mwanafunzi, mkulima na pia mwanzilishi wa chama kinachopiga vita unyanyasaji dhidi ya wanawake. Mariama anaungwa mkono na programu ya ITC ambayo ni taasisi tanzu ya Kamati ya Umoja wa Mataifa y
Screenshot/ITC

Camara Mariama Ciré: Mfano wa kuigwa kupitia kwenye kilimo Guinea Conakry 

“Habari, naitwa Camara Mariama Ciré kutoka Guinea Conakry…,” ndivyo anavyoanza Mariama Camara Cire kwa kujitambulisha kuwa anatokea Guinea Conakry moja ya nchi za Afrika Magharibi inayopakana na Bahari ya Atlantiki katika upande wake wa Magharibi na kwingine ikipakana na Guinea Bissau, Sierra Leone, Côte d'Ivoire, Senegal na Mali.