Ubaguzi wa kijinsia wachochea watoto wa kike kufeli hisabati- Ripoti
Kuelekea mkutano wa Umoja wa Mataifa wa Marekebisho ya Mfumo wa Elimu, Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto ulimwenguni UNICEF limetoa ripoti inayoonya kuwa viwango vya chini vya ustadi wa somo la hisabati hususani kwa wasichana, vinadhoofisha uwezo wa watoto hao kujifunza, kujiendeleza na kuwa na maendeleo.