Mafuriko ya Ziwa Albert Uganda yagharimu wilaya ya Buliisa dola 250,000
Mafuriko kwenye Ziwa Albert yamekuwa na madhara kwa uchumi kutokana na kutokea kwake wakati moja na mlipuko wa COVID-19 mwanzoni mwa mwaka 2020 hadi sasa Februari 2022.
Mafuriko kwenye Ziwa Albert yamekuwa na madhara kwa uchumi kutokana na kutokea kwake wakati moja na mlipuko wa COVID-19 mwanzoni mwa mwaka 2020 hadi sasa Februari 2022.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akizungumza na waandishi wa Habari baada ya kikao cha Baraza la Usalama kuhusu Ukraine amesema “Ingawa lengo letu halitajimia hatupaswi kukata tamaa. Ni lazima tuipe fursa amani na wanajeshi wanstahili kurejea makambini. Na viongozi kurejea kwenye njia ya majadiliano na amani.”
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa jioni hii limekutana kwa dharura kwa mara nyingine kujadili hali inayoendelea kutia wasiwasi mkubwa nchini Ukraine kwa lengo la kuiwajibisha Urusi kuzingatia kazuni na sheria za kimataifa lakini jitihada hizo zimegonga mwamba baada ya Urusi kuamua kwa mara nyingine kutumia tena kura yake ya turufu kupinga azimio lolote dhidi yake.
Mahakama ya Kimataifa ya Makoa ya Jinai (ICC) inaweza kuanza uchunguzi kuhusu vitendo vya mauaji ya halaiki, uhalifu dhidi ya ubinadamu na uhalifu wa kivita uliofanywa katika himaya ya Ukraine.
Shirika la Kimataifa la Nishati ya Atomiki (IAEA) limeeleza kuwa linafuatilia kwa wasiwasi mkubwa hali ya Ukraine.
Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula WFP limesema kimbunga Emnati kilichoikumba Madagascar Jumatano ya wiki hii (23/02/2022) kikiwa kimbunga cha nne kulikumba taifa hilo katika wiki kadhaa kinatishia uhakika wa chakula na ni mfano wa kjinsi gani cangamoto za mabadiliko ya tabianchi zisiposhughulikiwa zinaweza kusababisha mahitaji makubwa ya kibinadamu.
Ofisi ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa OHCHR imesema inatiwa wasiwasi mkubwa na hali inayoendelea Ukraine tangu jana mchana na usiku kucha ikipokea taarifa za raia kuuawa na wengine kujeruhiwa.
Umoja wa Mataifa umetenga dola za Marekani milioni 20 kutoka mfuko wake wa misaada ya dharura (CERF) ili kusongesha mara moja msaada wa kibinadamu wa kuokoa maisha na ulinzi kwa raia nchini Ukraine kufuatia ongezeko la hivi karibuni la mashambulizi.
Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Abdulla Shahid akizungumzia hali inayoendelea Ukraine, ametoa wito wa kusitishwa mapigano mara moja na kurejea katika diplomasia na mazungumzo.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amerejelea wito wake kwa Rais Viladmir Putin wa Urusi kurejesha majeshi yake nchini Urusi.