Mapigano mapya Jonglei, Sudan Kusini yafurusha maelfu ya watu
Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani Sudan Kusini, UNMISS umesema idadi ya familia zinazosaka hifadhi kwenye kituo chake huko Pibor jimboni Jonglei imeongezeka na kufikia 8,000 kufuatia mapigano mapya jimboni humo yaliyotokea tarehe 23 mwezi huu.