Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Sudan Kusini

Wajumbe wa baraza la usalama la Umoja wa Mataifa wakutana na rais wa Sudan Kusini Salva Kiir mjini Juba.
UNMISS/Isaac Billy

Sudan Kusini yatimiza miaka 9 ya uhuru inachokijua ni vita badala ya amani:UNHCR

Leo ni miaka tisa kamili tangu Sudan Kusini taifa changa kabisa duniani lijinyakulie uhuru baada ya kujitenga na Sudan. Lakini tangu lipate uhuru taifa hilo lilichokishuhudia ni vita zaidi ya amani, wimbi kubwa la wakimbizi na sasa linapambana na janga la corona au COVID-19 kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR.

Sauti
1'59"
Maafisa wa UNMISS wakizungumza na wenyeji katika soko lililoko mpakani
Video Screen Shot

Askari waliokuwa wanapigana, wameungana na wanakaribia kuhitimu mafunzo ya pamoja Sudan Kusini

Nchini Sudan Kusini, kufuatia kutiwa saini kwa makubaliano ya amani mnamo Septemba mwaka 2018, takribani askari 5000 kutoka makundi mbalimbali ambayo awali yalikuwa yanapigana, walichaguliwa ili kuwa sehemu ya kikosi kipya cha usalama wa kitaifa. Na sasa wanakaribia kuhitimu kabla ya kupangiwa kazi ya kulinda usalama katika maeneo mbalimbali nchini humo.

Sauti
2'15"