Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
Mapambano dhidi ya fistula, yanaweza kuathiriwa na janga la sasa la COVID-19-UN
Mapambano ya kutokomeza tatizo la fistula, moja ya majeraha ya hatari yanayotokea wakati wa kujifungua, yanaweza kuhatarishwa na janga la sasa la virusi vya corona au COVID-19, umetahadharisha ujumbe wa Umoja wa Mataifa kuhusu siku ya kimataifa ya kutokomeza fistula inayoadhimishwa kila tarehe 23 ya mwezi Mei kila mwaka.
Tujikwamue vyema tukilinda bayoanuwai baada ya COVID-19: Guterres
Kujikwamua kutoka kwenye janga la virusi vya corona au COVID-19 kunapaswa kwenda sanjari nan chi kuungana katika kulinda maliasili ya dunia hii kwa mujibu wa ahadi za kimataifa kwa lengo la kufikia mustakabali bora kwa watu wote na sayari dunia, amesema leo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa.
Wanandoa wakumbana na karaha badala ya raha, kisa? COVID-19
Katika mada kwa kina leo tunaelekea Uganda, kumulika mizozo ya kifamilia wakati huu wa mlipuko wa COVID-19 na madhara yake. Mizozo ambayo inadaiwa kusababishwa na wanafamilia kukaa pamoja majumbani kwa muda mrefu kutokana na vizuizi vya kutembea vilivyowekwa na serikali ikiwa ni moja ya hatua za kudhibiti kuenea kwa virusi vya corona. John Kibego anatupatia picha halisi.
COVID-19 inaongeza madhila ya kibinadamu Yemen:OCHA
Yemen nchi iliyoathirika vibaya na vita vya wenyewe kwa wewe sasa imeachwa ikabiliane na janga la virusi vya corona au COVID-19 na mfumo wa afya ambao umesambaratika na bila usaidizi zaidi wa kifedha limeonya leo shirika la Umoja wa Mataifa la misaada ya kibinadamu na masuala ya dharura OCHA.
Watu milioni 2.4 wahamishiwa kwenye makazi ya muda Bangladeshi kufuatia kimbunga Amphan
Kufuatia kimbunga Amphan kilichotua nchini Bangladesh wiki hii , wilaya 19 zimeathirika na watu zaidi ya milioni 2.4 wamelazimika kuhamishiwa kwenye makazi ya muda limesema leo shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula WFP.
COVID-19 huenda ikawatumbukiza watoto wengine milioni 10 katika utapiamlo:WFP
Janga la virusi vya corona au COVID-19 huenda likawatumbukiza watoto wengine milioni 10 zaidi katika utapiamlo uliokithiri kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na shirika la mpango wa chakula duniani WFP.
UN yazindua mikakati wa kupambana na taarifa potofu dhidi ya COVID-19
Umoja wa mataifa leo umezindua mpango wa kukabiliana na ongezeko kubwa la utoaji wa taarifa potofu kuhusu Ugonjwa wa virusi vya corona au COVID-19 kwa kuongeza kasi na ufikishwaji wa taarifa sahihi.
COVID-19 yaingia katika kambi ya Dadaab, Kenya na UNHCR zaimarisha huduma ya afya katika kambi za wakimbizi
Baada ya wagonjwa wawili wa virusi vya corona kuthibitishwa katika kambi ya wakimbizi ya Dadaab nchini Kenya, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR hii leo limetoa taarifa kuwa kwa kushirikiana na mashirika mengine ya kutoa msaada wa kibinadamu pamoja na serikali ya Kenya wanaimarisha mapambano yao dhidi ya COVID-19 katika kambi za wakimbizi nchini humo.
WHO na UNHCR washikamana kuimarisha afya ya wakimbizi na wasio na utaifa
Mashirika ya Umoja wa Mataifa la afya duniani WHO na lile la kuhudumia wakimbizi UNHCR leo yametia saini makubaliano mapya ili kuimarisha huduma za afya ya umma kwa mamilioni ya watu waliolazimika kukimbia makwao.
Guterres: Mshikamano na Afrika ni muhimu ili kusongesha maendeleo yaliyopatikana
Ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19 ukiendelea kusambaa barani Afrika, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amependekeza hatua za kisera za kusaidia bara hilo kukabiliana na changamoto zitokanazo na janga hilo ambalo hadi sasa limesababisha vifo vya watu 2500 barani humo.
Guterres ametoa mapendekezo hayo kupitia andiko lake la kisera huku akipongeza jinsi Afrika imechukua hatua haraka akisema kuwa ingawa idadi ya vifo hivi sasa ni ndogo kuliko ilivyodhaniwa , bado kuna mambo mengi yamesalia.