Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

Wanaharakazi vijana wakishiriki mgomo kwa ajili ya kuchagiza kuhusu mabadiliko ya tabianchi Stockholm, Sweden.
© UNICEF/Christian Åslund

Hatua zichukuliwe sasa kulinda mazingira la sivyo binadamu watageuka kafara: wataalam UN 

Miongo mitano baada ya kongamano la kwanza la dunia la kufanya mazingira kuwa suala kuu, wataalam wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa leo wametoa wito kwa mataifa kuongeza juhudi za kulinda sayari iliyo hatarini kwa ajili ya vizazi vya sasa na vijavyo huku kukiwa na changamoto ambazo hazijawahi kushuhudiwa za mazingira na nyinginezo.