Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

Wakulima nchini Rwanda na juhudi za kuimarisha ardhi.
© FAO/Petterik Wiggers

Njaa yashamiri Afrika, waathirika zaidi wakiwa ni Ukanda wa Afrika Mashariki

Idadi ya watu wenye njaa barani Afrika inaendelea kuongezeka, ikichochewa na uwepo wa migogoro, mabadiliko ya tabianchi na kuzorota kwa uchumi sababu nyingine mbalimbali ikiwemo pia janga la COVID-19. Imesema ripoti iliyotolewa leo na viongozi wa mashirika matatu ya kikanda barani Afrika ambayo  yametoa wito wa kuchukua hatua zaidi juu ya mabadiliko ya mifumo ya kilimo.

Sauti
1'56"