Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wafanyakazi wa kujitolea UM wana mchango mkubwa katika jamii

Wafanyakazi wa kujitolea UM wana mchango mkubwa katika jamii

Pakua

Leo ni siku ya kimataifa ya kujitolea ambayo kila mwaka huwa Desemba 5, kauli mbiu mwaka huu ni “jitolee chukua hatua kwanza”

Ni kijana Hussain Salim mratibu wa miradi na matukio kutoka Rally Tanzania Society, taasisi isiyo ya kiserikali inayohusika na shughuli za kujitolea na inafanya kazi kwa karibu na Umoja wa Mataifa nchini humo katika kusongesha mbele malengo ya maendeleo endelevu SDGs.

Umoja wa Mataifa unasema maelfu ya wafanyakazi wake wa kujitolea kama kijana Hussein wana mchango mkubwa, katika kusaidia kufanikisha ajenda ya umoja wa Mataifa ya maendeleo endelevu ya 2030 lakini pia malengo ya jamii wanakojitolea. Hussein ana ujumbe

 (Sauti ya Hussain Salim)

image
Hapa ni nchini Sudan Kusini, Solomon Ayiko (kulia) mfanyakazi wa kujitolea wa Umoja wa Mataifa akiwa kwenye doria na walinda amani kwenye njia inayotumiwa na wanawake kusaka kuni, eneo ambalo ni hatari zaidi kwa ukatili wa kingono na kijinsia.Pichani mkimbizi wa ndani akiwa amemshikilia Solomon ili asiteleze wanapopita kwenye njia hii yenye maji na madimbwi. (Picha:UNV/(Melanie Moore/ 2016)
Mbali ya mazingira wafanyakazi wa kujitolea wanashiriki katika masuala mengine kadha wa kadha. Sudan kwa mfano kuna wafanyakazi zaidi ya 200 wa kimataifa na kitaifa wanaojitolea kwenye mpango wa pamoja wa Umoja wa Mataifa na Muungano wa Afrika wa kulinda amani Darfur UNAMID, na baadhi ya shughuli wanazofanya ni kujenga barabara, kuwawezesha vijana, kuchagiza masuala ya haki za binadamu, kulinda watoto na kuchangia katika juhudi za kuleta amani na maendeleo .

Kwa mujibu wa Stuart J. Moran meneja wa mpango wa kujitolea wa Umoja wa Mataifa Darfur bila mchango wao kibarua kingekuwa kigumu.

(Sauti ya Stuart J. Moran)

"Watu wetu wa kujitolea wana jukumu muhimu sana la kusaidia jukumu kubwa la mpango wetu ambalo ni kulinda raia, hivyo tunapoona doria za UNAMID,   helkopta na kadhalika, vitu hivi haviwezi kufanyika bila msaada wa mfumo wa mfumo wa mpango wetu ikiwemo wafanyakazi wa kujitolea wa umoja wa Mataifa. "

 

Photo Credit
Stuart J. Moran maneja wa mpango wa kujitolea wa Umoja wa Mataifa Darfur UNAMID. Picha na UNAMID/Mohammad Mahady.