Hatimaye Umoja wa Mataifa hii leo umezindua ripoti yake ya mwisho ya maoni ya wakazi wa dunia kuhusu chombo hicho kinapotimiza miaka 75 tangu kuanzishwa kwake ambapo idadi kubwa kipaumbele chao cha muda mfupi ni huduma za msingi kama vile afya, elimu, maji na huduma za kujisafi, lakini pia matarajio yao na mawazo yao katika sula zima la ushirikiano wa kimataifa na kwa Umoja wa Mataifa kwa ujumla.