Jitolee muda wako wako, Jitolee kipaji chako, Jitolee uzoefu wako: Katibu Mkuu UN
Ikiwa leo ni Siku ya Kimataifa ya Kujitolea, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametoa wito kwa wanadamu kote duniani kutambua mchango wa wanaojitolea na pia kujifunza kutoka kwao ili kila mtu atoe mchango wa kutengeneza mstakabali mwema kwa watu wote.