Chuja:

UN-Tanzania

UN News/Patrick Newman

UN-Tanzania imefanya mengi kutuelimisha kuhusu SDGs- Rahma

Wiki hii katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani limefanyika kongamano la kimataifa la vijana la mwaka 2018, lenye lengo la kuwajumuisha vijana katika malengo ya maendeleo endelevu au SDGs.

Tulipata fursa ya  kukutana na mmoja wa washiriki wa jukwaa hilo Rahma Abdallah Mwita ambaye ni kijana kutoka Tanzania. Rahma ni mmoja wa wanzilishi wa mtandao  wa vijana kuhusu mabadiliko ya tabianchi ( Youth Climate Change Activist Network).

Sauti
5'22"

Wapatieni makazi ya kudumu wahamiaji 1,300 Libya- UNHCR

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR, limetoa  wito kwa serikali  zote duniani kutoa hifadhi wa kudumu kwa wahamiaji 1300 walioko katika mzingira magumu nchini  Libya.

Volker Turk  ambaye Kamisha msaidizi wa UNHCR kwa ajili ya ulinzi kwa wakimbizi amesema hali ya wahamiaji hao  nchini Libya ni ya kusikitisha sana, hivyo wahisani  wanahitajika kusaidia kuwapatia makazi ya kudumu.

Wafanyakazi wa kujitolea UM wana mchango mkubwa katika jamii

Leo ni siku ya kimataifa ya kujitolea ambayo kila mwaka huwa Desemba 5, kauli mbiu mwaka huu ni “jitolee chukua hatua kwanza”

Ni kijana Hussain Salim mratibu wa miradi na matukio kutoka Rally Tanzania Society, taasisi isiyo ya kiserikali inayohusika na shughuli za kujitolea na inafanya kazi kwa karibu na Umoja wa Mataifa nchini humo katika kusongesha mbele malengo ya maendeleo endelevu SDGs.