Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makala

UN/ Jason Nyakundi

Nchini Kenya vijana wabuni kifaa cha kunawa mikono kwa urahisi kujikinga na virusi vya Corona

Leo ni siku ya kimataifa ya vijana kaulimbiu mwaka huu ikiwa "ujumuishwaji wa vijana kwa ajili ya hatua za kimataifa" Umoja wa Mataifa ukisisitiza kuwa kundi hilo la watu katika jamii linaweza kuwa na mchango mkubwa katika kutatua changamoto zinazoikabili duniani hivi sasa. Nchini Kenya vijana wengi wameitikia wito wa kujumuishwa katika hatua za masuala ya kimataifa ikiwemo vita dhidi ya janga la corona au COVID-19 ambalo linaendelea kuitikisa dunia kwa sasa.

Sauti
5'27"
UN Tanzania/Ahimidiwe Olotu

Asante UNIC Dar es Salaam kunipa fursa ya kukuza maarifa yangu-Hilda Amedhastone Phoya

Je una ndoto za siku moja kufanya kazi na Umoja wa Mataifa? Makala ifuatayo ni mahojiano kati ya Ahimidiwe Olotu wa UNIC Dar es Salaam na Hilda Amedhastone Phoya, mwanafunzi ambaye amehitimisha mafunzo kwa vitendo katika Kituo cha habari cha Umoja wa Mataifa UNIC Dar es Salaam, akieleza kuhusu alivyonufaika na fursa ya kujifunza kwa vitendo katika kituo hicho kinachohusika na habari za Umoja wa Mataifa nchini Tanzania na jinsi kituo hicho kilivyonoa uelewa wake kuhusu masuala mbalimbali ya kimataifa. 

Audio Duration
3'39"
UNEP/Natalia Mroz

Wanyama wahatarisha usalama wa chakula kati nya COVID-19, Uganda

Wanyama ni sehemu muhimu ya mazingira na pia uwepo wao hutegemea mazingira sawa na binadamu. Lakini uchafuzi wa mazingira kutokana na ongezeko la idadi ya watu na baadhi ya watu kutojali maana ya misitu na maeneo mengine, makaazi ya wanyama yamechafuliwa na kuchochea mzozo kati ya binadamu na wanyama ambapo uhakika w achakula umeigia hatarini zaidi hasa kwa jamii jirani za mbuga za wanyamapori nchini Uganda.

Sauti
3'50"
Picha ya IFAD

Mzee ajikwamua kwa kujiimarisha katika kilimo cha pilipili, Uganda

Katika juhudu za binafsi za kufikia lengo namba moja la malengo ya maendeleo endelevu au SDGs, mzee mmoja nchini Uganda ameamua kujikwamua kutoka katika lindi la umaskini kwa kujiimarisha katika kilimo cha pilipili.

Mzee Jacob Byemaro wa kijiji cha Bulima tarafa ndogo ya Bwijanga wilayani Masindi, ameamua kurejelea upanzi wa mazao yanayohitaji nguvu kazi kidogo lakini yakitoa mavuno yenye thamani kubwa sokoni.

Sauti
3'40"
World Bank/Sue Pleming

Hali ya hewa ya Morogoro haikuwa hivi, hatua za pamoja na za haraka zinahitajika-Wakazi wa Morogogo

Mkoa wa Morogogoro ulioko katika eneo la mashariki la Tanzania ni moja ya maeneo ambayo kwa miaka mingi yametambulika kuwa maeneo yenye hali nzuri ya hewa kutokana na mazingira yake kuwa yenye misitu, nyika, na milima yenye kutiririsha maji safi. Lakini katika miaka ya hivi karibuni wanaharakati wa kutunza mazingira wanaona kuwa ni muhimu kuchukua hatua za kuilinda hali hiyo kwani iko katika hatari ya kutoweka kutokana na shughuli za binadamu kama vile uchomaji mkaa.

Audio Duration
3'36"
UN/Assumpta Massoi

Matembele 'shata' au matembele afya?

Huko visiwani Zanzibar nchini Tanzania katika eneo la Kidoti, Wilaya ya Kaskazini A, mafunzo  yaliyotolewa na chama cha wanahabari wanawake Tanzania, TAMWA visiwani humo yamekuwa na manufaa makubwa kwa wanakikundi cha Mwanzo Mgumu. Mafunzo hayo kuhusu masuala ya kilimo na ufugaji yamesaidia kuimarisha afya za watoto ambao awali mama zao walikuwa na uelewa mdogo kuhusu jinsi ya mapishi ya mboga. Wengi walizoea kupika matembele 'shata' wakimaanisha kuchemsha matembele kwa muda mrefu na kisha kutumia tui la nazi. Lakini mafunzo yaliwawezesha kutambua umuhimu wa matembele yenye afya.

Sauti
4'1"