Makala yenye kuangazia siku ya urafiki duniani
Tarehe 30 Julai, jamii ya kimataifa imeadhimisha siku ya urafiki duniani, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa akisema urafiki hujenga daraja baina ya watu, na hivyo huchochea amani duniani. Kwenye ujumbe wake kwa siku hiyo, Bwana Ban amesema urafiki ni muhimu sana kwenye dunia ya leo inayokumbwa na ubaguzi, ukatili na mizozo inayoathiri mamilioni ya watu.