Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari kwa Ujumla

Delight Uganda Limited

Biashara ya kilimo kiganjani nchini Uganda

Ubia kati ya kampuni binafsi ya huduma za malipo kwa njia ya simu, MobiPay nchini Uganda na kituo cha Umoja wa Mataifa cha biashara, ITC umeondoa usumbufu wa malipo kwa wakulima baada ya mauzo yao na hata kuwajengea mbinu ya kisasa zaidi ya kujiwekea akiba ya fedha badala ya kuzitumia kiholela baada ya mauzo. Grace Kaneiya  na maelezo zaidi. 

Sauti
2'4"
© UNICEF/Jean-Claude Wenga

Tulisikia mitetemo na moto kila mahali na tukakimbia- Manusura wa volkano ya Nyiragongo, DRC

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR na wadau wengine wanawasaidia watu waliolazimika kuyakimibia makazi yao baada ya mlipuko wa volkano katika Mlima Nyiragongo nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, DRC. Wengi walivuka mpaka kwenda nchi jirani ya Rwanda ambako sasa wanapata usaidizi. Taarifa ya Assumpta Massoi inaeleza zaidi.
Huyu ni Joyce, raia kutoka DRC ambaye amekimbilia hapa Rubavu nchini Rwanda akisimulia alichoshuhudia huko kwao jimboni Kivu Kaskazini ambako volkani kutoka mlima Nyiragongo ilianza kulipuka tarehe 22 mwezi uliopita wa Mei.

Sauti
2'21"
UN Photo/Eskinder Debebe)

Pamoja na kuifunga ofisi ya Mjumbe Maalum wa Katibu Mkuu, UN yaahidi kuendelea kuisaidia Burundi

Baada ya miaka minne ya shughuli nchini Burundi, Ofisi ya Mjumbe Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Burundi, OSESG-B imefungwa rasmi jana Mei, 30, 2021.  Harumukiza Edmond wa televisheni washirika, Mashariki TV ana maelezo zaidi.

Sherehe hiyo rasmi imeongozwa na Mjumbe Maalum wa Katibu Mkuu wa Kanda ya Maziwa Makuu, Bwana Huang Xia. Maafisa wakuu wa Serikali, wawakilishi wa vyama vya kisiasa na asasi za kiraia, wanachama wa Jumuiya ya kidiplomasia, na wakuu wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na wengine, wamehudhuria tukio hilo. 

Sauti
2'37"
© UNICEF/Henry Bongyereirwe

Asante UNICEF kutufungulia ukurasa mpya wa maisha:Yatima Uganda

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF kwa msaada wa serikali ya Japan limefungua mlango wa maisha mapya kwa watoto yatima waliopoteza matumaini baada ya kifo cha mama yao. Paul na Florence miaka sita iliyopita waliachwa yatima na bila makazi ya kuaminika na bila chochote mama yao alipofariki dunia kwa ukimwi katika wilaya ya Kabale nchini Uganda lakini leo hii wanasema makazi mapya waliyojengwa na UNICEF ni ukurasa mpya wa maisha yao. John Kibego anasimulia zaidi  

 (TAARIFA YA JOHN KIBEGO)  

Nattss…… 

Sauti
2'40"
© UNICEF/Ismail Taxta

Tusipolinda afya kila kitu kipo hatarini: WHO

Baraza la Afya duniani, limehitimisha kikao chake cha 74 kwa kupitisha azimio la kihistoria la kuimarisha utayari wa uwajibikaji wa shirika la afya ulimwenguni -WHO pindi dharura inapotokea. Assumpta Massoi na maelezo zaidi. 

(Taarifa ya Assumpta Massoi) 

 Baraza hilo limepitisha azimio hilo huku Mkurugenzi Mkuu wa WHO, Dkt.Tedros Ghebreyesus, akipongeza nchi wanachama, kwa kupunguza vifo vitokanavyo na COVID-19 na kuonya litakuwa kosa kubwa iwapo watafikiri hatari ya janga hilo imeondoka. 

Sauti
2'39"