Athari za mabadiliko ya tabianchi ni 'mwiba' kwa watoto- UNICEF
Mwakilishi wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF, nchini Msumbiji Maria Luisa Fornara akitembelea eneo la Guara Guara ambayo sasa ni makazi ya walioathiriwa na kimbunga Eloise, amesema inasikitisha kuona watoto wakiteseka kwa mara nyingine kutokana na matokeo mabaya ya mabadiliko ya tabianchi. Grace Kaneiya na maelezo zaidi.