Kampuni ya Mars na IFAD zachukua hatua kunusuru wakulima wa kakao na walaji wa chokoleti
Mfuko wa kimataifa wa ufadhili wa ajili ya kilimo IFAD na kampuni kubwa ya kutengeneza chokoleti duniani Mars zimeshikamana kuchukua hatua kukabiliana na uhaba wa zao la kakao ambalo ni kiungo muhimu katika utengenezaji wa kiburudisho kinachopendwa kila kona ya dunia, chokoleti.
Chokoleti moja ya viburudisho vinavyopendwa na watu wengi duniani zinapatikana katika maumbo na mchanganyiko wa kila aina lakini ili ziendelee kutengenezwa zinahitaji kiungo muhimu ambacho ni zao la kakao.