Guterres awasiliana na AU kuhusu sakata nchini Zimbabwe
Kufuatia sintofahamu inayoendelea hivi sasa nchini Zimbabwe, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema anafuatilia kwa karibu kinachoendelea huku akisihi utulivu.
Vyombo vya habari vinaripoti kuwa hivi sasa jeshi nchini Zimbabwe limeshika hatamu huku Rais Robert Mugabe akiwa ameshikiliwa ndani ya nyumba yake.
Kupitia msemaji wake Stephane Dujarric ambaye amezungumza na waandishi wa habari leo jijini New York, amesema wana wasiwasi mkubwa na kile kinachoendelea na hivyo Katibu Mkuu ..
(sauti ya Dujarric)