Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari kwa Ujumla

Guterres awasiliana na AU kuhusu sakata nchini Zimbabwe

Kufuatia sintofahamu inayoendelea hivi sasa nchini Zimbabwe, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema anafuatilia kwa karibu kinachoendelea huku akisihi utulivu.

Vyombo vya habari vinaripoti kuwa hivi sasa jeshi nchini Zimbabwe limeshika hatamu huku Rais Robert Mugabe akiwa ameshikiliwa ndani ya nyumba yake.

Kupitia msemaji wake Stephane Dujarric ambaye amezungumza na waandishi wa habari leo jijini New York, amesema wana wasiwasi mkubwa na kile kinachoendelea na hivyo Katibu Mkuu ..

(sauti ya Dujarric)

Kikosi cha kikanda Sudan Kusini kukamilika mwishoni mwa mwaka huu- UNMISS

Kikosi cha ulinzi cha kikanda, RPF, kinachopelekwa nchini Sudan Kusini kitakuwa kimekamilika ifikapo mwisho wa mwaka huu.

Mwakilishi maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini, David Shearer amesema hayo hii leo akizungumza na waandishi wa habari kwenye mji mkuu Juba, akigusia kikundi hicho kinachoundwa na askari kutoka nchi za Afrika.

Amesema kikosi hicho kilichoidhinishwa na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kitakuwa na jumla ya askari 4,000.

(Sauti ya David)

Usaidizi waendelea kwa manusura wa tetekemo la ardhi Iran na Iraq

Shirika la afya ulimwenguni, WHO limeendelea kupeleka vifaa vya matibabu kwa manusura wa tetemeko la ardhi mpakani mwa Iran na Iraq.

Vifaa vya hivi karibuni zaidi ni vile vya kusaidia matibabu ya maelfu ya watu waliojeruhiwa na kukumbwa na kiwewe baada ya mkasa huo wa jumapili jioni.

Mkurugenzi wa WHO anayehusika na masuala ya dharura kwenye ukanda huo Dkt. Michel Thieren amesema vifaa hivyo vitatosheleza matibabu kwa watu 4,000 na misaada zaidi inasafirishwa kutoka bohari ya shirika hilo huko Dubai, Falme za Kiarabu.

WFP,UNICEF,WHO watoa ombi kuondoa vizuizi vya misaada ya kibinadamu Yemen

Wakuu wa mashirika ya Umoja wa Mataifa leo wametoa ombi lingine la pamoja la kutaka kuondolowa haraka vikwazo ili kufikisha misaada ya kibinadamu kwa mamilioni ya watu walio hatarini Yemen.

Wakuu hao wa shirika la mpango wa chakula duniani WFP, la kuhudumia watoto UNICEF na la afya duniani WHO wamesema vizuizi hivyo vya anga, baharini na nchi kavu vimeifanya hali ya Yemen ambayo tayari ilikuwa mbaya kuwa janga kubwa na baya zaidi la kibinadamu duniani.

Mkakati wa kimataifa wa bima wazinduliwa kukabili mabadiliko ya tabia nchi:Thiaw

Mkakati wa kimataifa wenye lengo la kutoa bima kwa watu wasiojiweza na masikini zaidi ya milioni 400 ifikapo mwaka 2020 umezinduliwa leo mjini Bonn Ujerumani.

Mkakati huo “bima ya mnepo kwa ajili ya mabadiliko ya tabia nchi na hatari ya majanga umeziduliwa wakati wa mkutano unaoendelea wa mabadiliko ya tabia nchi COP23 , ukizileta pamoja nchi tajiri za G20 kushirikiana na nchi 20  zilizo katika hatari zaidi au V20.