WHO yafikisha misaada ya kibinadamu Syria
Shirika la Afya Duniani, WHO, limewasilisha zaidi ya tani 11 za vifaa vya matibabu kwa mamlaka za afya katika eneo la Al-Qamishli, kaskazini mwa Syria.
Taarifa ya WHO imesema hii ni mara ya kwanza kwa WHO kusafirisha kwa njia ya anga hadi eneo hilo vifaa vya matibabu tangu mwaka jana.
Vifaa hivyo ni pamoja na dawa za huduma za dharura, dawa za magonjwa yasiyo ya kuambukiza, tembe za dawa za maumivu, virutubisho vya lishe pamoja na viti mwendo.