Mamia ya wakimbizi wa Ivory Coast na Angola warejea nyumbani:IOM
Mamia ya wakimbizi ambao walihama makwao kutokana na mzozo wa uchaguzi ulioikumba Ivory Coast wameanza kurejea nyumbani kwa usaidizi wa shirika la kimataifa la uhamiaji IOM.
Mamia ya wakimbizi ambao walihama makwao kutokana na mzozo wa uchaguzi ulioikumba Ivory Coast wameanza kurejea nyumbani kwa usaidizi wa shirika la kimataifa la uhamiaji IOM.
Shirikisho la kimataifa la maradhi ya Kisukari IDF na shirika la afya duniani WHO wanasema maradhi ya kisukari yanaweza kuzuuilika kwa watu kuzingatia masharti ikiwemo kula vyakula vinavyofaa, kufanya mazoezi, kupungza unene na kuepuka matumizi ya tmbaku.
Shirika la maendeleo la Umoja wa Mataifa UNDP limezindua ripoti ya maendeleo ya binadamu mwaka 2011 nchini Tanzania. Washirika mbali mbali walihudhuria mkutano huo wakiwemo Dr Paniel Lyimo, katibu mkuu wa kudumu kwenye ofisi ya waziri mkuu wa Tanzania ambaye alikuwa mgeni rasmi, Dr.
Mwakilishi maalmu wa Umoja wa Mataifa nchini Somalia balozi Augustine Mahiga amesema ana matumaini operesheni za pamoja za kijeshi za serikali ya mpito na Kenya dhidi ya wanamgambo wa Al-Shabaab zikikamilika hali ya amani itakuwa shwari Somalia.
Huko Burundi, Jeshi la nchi hiyo limesema kwamba halitavunjika moyo licha ya tukio la hivi karibuni nchini Somalia ambako walinda amani wake katika kikosi cha Amisom waliuwawa wiki iliopita. Hata hivo giza linaendelea kutanda kuhusu idadi ya wanajeshi waliouwawa.
Mwakilishi maalumu wa Umoja wa Mataifa nchini Somalia Balozi Augstine Mahiga leo amethibitisha kwamba vikosi vya jeshi la Kenya vimeingia Somalia.
Serikali ya Tanzania imeitaka jumuiya ya kimataifa kuongeza juhudi na kunyoosha mkono zaidi kusaidia kunusuru maisha ya mamilioni ya watu nchini Somalia.
Nchi nyingi zinazoendelea bado hazijamudu kukabiliana na athari za majanga ya asili na hata yanayosababishwa na shughuli za binadamu. Hayo yamesemwa na Umoja wa Mataifa katika kuadhimisha siku ya kimataifa hii leo ya kupunguza majanga.
Shirika la kimataifa la uhamiaji IOM linasaidia maelfu ya raia wa Sudan Kusini kurejea nyumbani.
Kwa mujibu wa shirika hilo maelfu ya raia hao wengi walikuwa wamekwama katika eneo la Kosti na wengine ni wale walioishi Kaskazini kwa muda na sasa wanataka kurudi nyumbani.