Heko Uganda kwa kuwaenzi wakimbizi:UNHCR
dailynews023c-18_01Kamishina mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR, ameipongeza serikali ya Uganda kwa sera nzuri isiyokuwa na mipaka wala urasimu inayowaenzi na kuwathamini wakimbizi wanaoingia nchini humo. Tupate maeelezo kamili na Joseph Msami
Akiwa ziarani nchini Uganda,kamishina Filopo Grandi akizungumza na wandishi wa habari, amesema Uganda ni nchi pekee Afrika na hata duniani iliyo na sera nzuri zisizobagua wakimbizi kwenye mipaka yake na ni nchi pekee iliyotoa hifadhi kwa zaidi ya wakimbizi milioni 1.4.
(SAUTI YA FILIPPO GRANDI)
“Napenda kuchukua fursa hii kuishukuru, Serikali ya Uganda, sana sana na wananchi wa eneo hili kwa kuendelea kuwapokea wakimbizi. Uganda inapokea zaidi ya wakimbi 500 kwa siku, wengi wao wakitoka Sudan Kusini na Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo na ukanda wa madharibi. Wengi wanakuja Uganda kwasababu ya sera nzuri na mapokezi mazuri ya serikali ya Uganda.
kwa sasa kambi za Impvepi na Rhino zilizopo katika wilaya ya Arua kuna takribani wakimbizi 245, 000 wengi wao wakitoka Sudani Kusini na kupewa hifadhi na ardhi kwajili ya kilimo na shughuli zingine za maendeleo.
Aidha bwana Grandi ametoa wito kwa serikali ya Uganda kuendelea na sera hiyo ambayo huleta maendeleo katika sekta ya kilimo, miundombinu na pia ajira kwa wenyeji .
Katika ziara yake mkuu huyo wa UNHCR alikutanda na waziri mkuu wa Uganda Bwana Ruhakana Rugunda na kutoa shukrani kwa niamba ya Umoja wa Mataifa na kuahidi ushirikiano zaidi baina ya UNHCR na serikali ya Uganda katika kutafutia mwafaka swala la huduma kwa ukimbizi katika eneo la maziwa makuu.