Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kongamano la kimataifa la takwimu na uhamiaji lang’oa nanga Paris:IOM

Mkurugenzi Mkuu wa IOM William Lacy Swing (kulia) katika kongamano la kimataifa la takwimu na uhamiaji lililoandaliwa kwa pamoja na IOM, OECD na UNDESA, ambalo lilianza leo (15/01) huko Paris. Picha: OECD

Kongamano la kimataifa la takwimu na uhamiaji lang’oa nanga Paris:IOM

Shirika la  Umoja wa Mataifa la  Uhamiaji IOM kwa ushirikiano na idara ya mambo ya uchumi  na kijamii  ya Umoja wa Mataifa UNDESA na shirika la ushirikiano wa maendeleo na uchumi OECD leo wameanza kongamano mjini Paris Ufaransa kuhusu ukusanyaji takwimu za uhamiaji duniani. Tupate tarifa zaidi na Patrick Newman

(TAARIFA YA PATRICK)

Kongamano hilo la siku mbili, lilofungiliwa na bwana Wiliam Lacy ni mkurugenzi mkuu wa IOM, Liu Zhenmin, katibu mkuu wa UNDESA na  bi Angel Gurria katibu mkuu wa shirika la ushirikiano wa maendeleo na uchumi OECD pia  limewaleta pamoja zaidi ya watalamu 700 wa maswala ya kukusanya takwimu duniani, asasi za kiraia na watunga sera ili kujadili swala  la uhamiaji  ambalo kwa sasa ni jambo mtambuka katika kila pembe ya duniani.

Bwana Swing wa IOM amesema , bila kuwepo na takwimu zinazoaminika ni vigumu kuweka bayana será na miongozo itakayowezesha kukabiliana na tatitzo la uhamiaji duniani.

Kongamano hilo ltakalo jadili pia mtitazamo na maoni ya watu na wenyeji katika nchi zinazopokea wahamiaji limepangwa kufanyika mara mbili kwa mwaka, kwa ushirikiano na mashirika mbalimbali yakijumuisha shirika la kazi duniani  ILO, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudmia wakimbizi UNHCR,shirika la Umoja wa Mataifa la uhalifu na madawa UNODC, Eurostat na tume ya Umoja wa Mataifa ya maendeleo ya uchumi barani Ulaya UNECE,  kama jukwaa la kukusanya takwimu na pia kujadili mikakaki ya maswala la uhamiaji duniani.