Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Simulizi ya mtoto Ahmed aliyenusurika vitani Iraq

Simulizi ya mtoto Ahmed aliyenusurika vitani Iraq

Baada ya mazonge ya vita, manusura huathirika kwa namna kadhaa ikiwamo kiuchumi, kijamii na hata kisaikolojia. Hili liko dhahiri nchini Iraq ambapo mapigano kati ya vikosi vya serikali na kundi la kigaidi la ISIL yanaendelea.

Katika makala ifuatayo Rosemary Musumba anamulika juhudi za kuwasaidia vijana baada ya athari za kivita nchini humo ambapo Umoja wa Mataifa kushirikiana na wadau unatoa usaidizi wa kijami na kisaikolojia, ungana naye.