Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Mahojiano

UN News

EAC yasisitiza usalama, uchumi na masuala ya kidijitali katika Mjadala Mkuu wa UNGA80

Kama unavyofahamu Mjadala Mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa UNGA80 umekunja jamvi rasmi  jana Jumatatu. Na tumepata fursa ya kuzungumza na washiriki mbalimbali akiwemo Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki EAC, Veronica Nduva ambaye alizungumza na Flora Nducha kandoni mwa mjadala huo kuangazia mchango wa Jumuiya ya Afrika Mashariki katika kutekeleza ajenda ya Umoja wa Mataifa ikiwemo masuala ya Amani na usalama, maendeleo na ushirikiano wa kikanda. Ungana nao.

Sauti
9'11"
Photo: Una Smith

Chokoleti itengenezwayo Uganda yavuka mpaka na mabara -UNCTAD

Kutoka kakao ghafi huko Bundibugyo, magharibi mwa Uganda hadi Kampala mji mkuu wa kibiashara wa taifa hilo la Afrika Mashariki ndiko kunapatikana kiwanda cha kutengeneza chokoleti cha Equator kinachomilikiwa na Barbara Gonget na mume wake Gustav. Awali wazo la biashara hii lilionekana kutokuwa na mashiko. Ingawa hivyo baada ya ITC, ambacho ni Kituo cha Kimataifa ha Biashara kilicho chini ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Biashara na Maendeleo, UNCTAD pamoja na wadau wao kuweka usaidizi wao, hali imebadilika na sasa biashara inavuka sio tu mipaka bali mabara.

Sauti
3'55"
UN News/Sharon Jebichii

Kutimiza azimio la watu wa jamii za asili ni jukumu la mataifa yote duniani - Adam Ole Mwarabu

Jukwaa la Umoja wa Mataifa kuhusu watu wa jamii za asili limekunja jamvi mwishoni mwa wiki iliyopita hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa na kandoni mwa jukwaa hilo Flora Nducha wa Idhaa hii ya Kiswahili alipata fursa ya kuzungumza na mmoja wa washiriki kiongozi wa kijamii kutoka Jamii ya wafugaji ya Wamaasai mkoani Morogoro Mashariki mwa Tanzania Adam Kulet Ole Mwarabu, wamejadili mengi lakini Ole Mwarabu anaanza kwa kukumbusha alichokibeba kwenye jukwaa la mwaka jana kinavyotekelezwa nchini mwake.

Sauti
6'48"
UN Video

Chata ya Umoja wa Mataifa inasongesha amani, maendeleo, urafiki na haki za binadamu - Balozi Yabesh Monari

Tarehe 25 mwezi Aprili kila mwaka ni siku ya kimataifa ya wajumbe wanaowakilisha nchi zao kwenye Umoja wa Mataifa. Tarehe hiyo mwaka 1945 ndio ulianza mkutano huko San Francisco, Marekani wa wajumbe 850 kutoka nchi 50 waliopitisha Chata ya Umoja wa Mataifa ikilenga kusongesha amani, maendeleo, urafiki na haki za binadamu. Kama unavyofahamu Umoja wa Mataifa sasa umekua na idadi ya wanachama ni 193 na kila moja hupeleka wawakilishi kufanikisha utekelezaij wa malengo ya Umoja huo. Lengo la siku ni kuwatambua kwani wao ndio wamepewa jukumu la kufanikisha chata hiyo.

Sauti
6'42"
UN News/Sharon Jebichii

Zanzibar tumetekeleza kwa vitendo azimio la Beijing: Waziri Riziki Pembe

Wakati mkutano wa 69 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake Duniani CSW69 ukifikia ukingoni mshiriki kutoka Zanzibar Tanzania ameweleza Flora Nducha wa Idhaa hii ya Kiswahili kwamba Zanzibar imepiga hatua kubwa katika usawa wa kijinsia na utekelezaji kwa vitendo matakwa ya Azimio la Beijing la usawa wa kijinsia na hatua. Je wametekeleza vipi na hatua gani walizopiga? Ungana nao katika mahojiano haya.

Sauti
5'39"
United Nations

UNESCO na wadau wanajitahidi kuboresha elimu licha ya mashambulizi dhidi ya elimu katika migogoro.

Kama unavyojua, migogoro ya vita, majanga ya tabia nchi, dharura za afya ya umma, na mishtuko ya kiuchumi inaongezeka duniani kote kwa kasi, ugumu, na ukubwa. Mara nyingi dharura hizi hutokea kwa wakati mmoja, kwa mfano, wakati vita vinapoanza katika maeneo ambayo tayari yameathiriwa na majanga ya mabadiliko ya tabianchi. Hali hii inasababisha migogoro tata, iliyo changamana na ya muda mrefu, na athari zake kwenye elimu ni za kutisha. Nafikiri utakubaliana nami kuwa elimu ni mkombozi wa maisha na muhimu kwa kuendeleza maisha wakati wa dharura. Je UNESCO inatatua vipi changamoto hii?

Sauti
4'27"
UN News/Bosco Cosmas

Je wewe ni mmoja wa waathirika wa usugu wa viuavijiumbe maradhi, au Usugu wa Vimelea dhidi ya Dawa, UVIDA?

Leo hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa, kando ya mjadala mkuu wa UNGA79, viongozi wanakutana kwenye Mkutano wa Ngazi ya Juu ukimulika usugu wa viuavijiumbe maradhi, Antimicrobial Resistance, kwa kiswahili ikiitwa pia UVIDA, au Usugu wa Vimelea dhidi ya Dawa. Katika taarifa ya Pamoja iluyotolewa kwenye mkutno huo na mashirika ya Umoja wa Mataifa lile la afya duniani WHO, la mazingira UNEP, la chakula  na kilimo FAO na shirika la afya ya Wanyama duniani WOAH, usugu wa viua vijiumbe maradhi unahusika moja kwa moja na vifo milioni 1.3 na kuchangia vingine milioni 5 kila mwaka.

Sauti
6'16"
UN News

Vijana - Tumechoka na maneno ya viongozi sasa tunataka vitendo

Jana Jumapili ya Septemba 22 viongozi wa dunia walipitisha Mkataba wa Zama Zijazo. Mkataba huu unalenga kukabili changamoto za karne ya 21 kuanzia mizozo, mabadiliko ya tabianchi, haki za binadamu, hadi taarifa potofu na za uongo. Maeneo Matano makuu ni pamoja na maendeleo endelevu, amani na usalama duniani, sayansi na teknolojia, vijana na vizazi vijavyo na marekebisho ya usimamizi wa dunia, kipengele muhimu wakati huu ambapo taasisi za fedha za kimataifa na Umoja wa Mataifa wenyewe wameshindwa kuja na majawabu ya karne ya 21.

Sauti
7'27"