Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Azimio lapitishwa kuanzisha fuko la dunia dhidi ya vijiuadudu

Azimio lapitishwa kuanzisha fuko la dunia dhidi ya vijiuadudu

Mkutano kuhusu usugu wa dawa dhidi ya vijiuadudu umetamatishwa kwa wajumbe kupitisha nyaraka ambayo pamoja na mambo mengine inataka kuwepo kwa fuko la dunia, au Global Fund litakalosongesha harakati za kudhibiti usugu huo.

Imeelezwa kuwa dawa dhidi ya vijiuadudu zimeonekana kuwa sugu kwa binadamu, mifugo na hata mashambani ambapo wajumbe wamesema inahatarisha mipango ya kufanikisha malengo ya maendeleo endelevu, SDGs.

Kenya ni moja ya nchi zilizowasilisha muswada wa kudhibiti usugu wa vijiuadudu ambapo Waziri wake wa Afya, Dkt. Cleopa Mailu ameiambia Idhaa hii kuwa fuko hilo la dunia litarahisisha mafunzo, udhibiti na utafiti dhidi ya usugu huo kwa kuwa...

(Sauti ya Dkt. Mailu)

Kwa hiyo amesema ..

(Sauti ya Dkt. Mailu)