Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Kikao cha 71 cha Baraza Kuu

Kikao cha 71 cha baraza Kuu kimefunga pazia:

Kikao cha 71 cha baraza kuu la Umoja wa Mataiofa leo kimefunga pazia kwenye makao makuu ya Umoja huo hapa New york Marekani. Akizungumza katika mkutano wa ufungaji wa kikao hicho Katibu Mkuu wau moja wa Mataifa Antonio Guterres amemshukuru Rais wa kikao cha 71 Peter Thompson kwa kazi nzuri aliyoifanya kwa mwaka mzima

(GUTERRES CUT 1)

Zahma na vita vyahatarisha uhakika wa chakula

Shirika la Chakula na Kilimo, FAO limesema nchi 39 ulimwenguni zinategemea msaada wa chakula kutokana na vita na majanga ya asili.

FAO imesema hayo katika ripoti yake iliyotolewa Alhamisi iitwayo "Matarajio ya mazao na hali ya chakula", ikitaja Cameroon na Chad kuwa miongoni mwao na hilo limesababishwa na kulemewa na idadi kubwa ya wakimbizi kutoka nchi jirani.

Halikadhalika imetaja Sudan Kusini ambapo migogoro mikubwa imekwamisha shughuli za kilimo wakati nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati mapigano yameleta hasara na upungufu wa rasilimali katika kaya.

UN Photo/Paulo Filgueiras

Jopo huru lichunguze mauaji ya wamarekani weusi- Wataalamu

Jopo la wataalamu wa haki za binadamu la Umoja wa Mataifa limetaka kufanyika uchunguzi huru dhidi ya mauaji ya wamarekani weusi yanayofanywa kinyume cha sheria na polisi huko Marekani.

Wataalamu hao wanaojikita katika watu wenye asili ya Afrika wametoa wito huo kufuatia mauaji ya Keith Scott huko jimbo la Carolina Kaskazini wakitaka uchunguzi huo ufanywe na watu wasiowajibika kwa serikali ya Marekani.

Ricardo Sunga ni mkuu wa jopo hilo.

(Sauti ya Ricardo)