Diamond, SautiSol waungana na wenzao #SDGs: VIDEO
Malengo ya maendeleo endelevu, SDGs au #Globalgoals yanapitishwa baadaye mwezi huu. Kupitia kampeni ya Global Gloals Africa campaign, wanamuziki wa Afrika wakiwemo SautiSol, Diamond, Yemi Alade na wengineo wakajumuishwa katika uimbaji wa kibao hiki kikiwa na lugha ya kiswahili, kiingereza, kitoofan, kizulu na kifaransa. Ungana nao wakielezea umuhimu wa malengo hayo 17. Kampuni ya Unilever ndiyo ilifadhili video hii.