Ban apongeza IGAD kwa hatua za kukomesha mgogoro Sudan Kusini
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Moon amepongeza misimamo imara iliyopitishwa na wakuu wa nchi wanachama wa jumuiya ya maendeleo IGAD kuhusu mgogoro wa Sudan Kusini kwa maslahi ya wananchi
Tarifa ya msemaji wa Katibu Mkuu inasema ametiwa moyo na dhamira ya pande kinzani kusitisha mapigano na kufikia makubaliano kuhusu mgawanyo wa madaraka jumuishi ndani ya siku 15.
Imemnukuu Bwana Ban akisema ana matumaini kuwa pande hizo zitasimamia ahadi zao kuhusu amani na kujihusisha katika majadiliano kwa dhati ili kufikia makubaliano ya kina ya amani yatakayoshughulikia chanzo cha mgogoro Sudan Kusini