DRC: Watoto 12 waliokuwa wanatumishwa Kivu Kaskazini waokolewa- MONUSCO
Huko nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO umeendelea kuunga mkono juhudi za serikali za kujumuisha kwenye jamii wapiganaji wa zamani, hatua inayofanyika kupitia programa ujumbe huo ya Kupokonya silaha, Kuvunja Makundi na Kujumusha wapiganaji kwenye jamii, PDDRCS.