Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Mamilioni ya watu kote ulimwenguni wanapoanza kuadhimisha mwezi Mtukufu wa Ramadhani, kwa huzuni huko Gaza na katika eneo lote, wengi wataadhimisha mwezi huu wakikabiliwa na migogoro, kufukuzwa na hofu.
© UNRWA

Ni wakati wa Ramadhan tusitishe uhasama Gaza na Sudan: Guterres

Leo ni mwanzo wa mwezi mktukufu wa Ramadhan ambapo Waislamu kote duniani hudumisha na kuchagiza tunu za amani, maridhiano na mshikamano lakini uhasama unaendelea hususani sehemu mbalimbali duniani ikiwemo Gaza ambako mauaji , na mashambulizi hayajakoma amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akizungumza na waandishi wa habari mjini New York Marekani hii leo. 

Sauti
2'53"
Huduma za kibinadamu na haki za binadamu zazidi kutwama nchini Haiti..
© UNICEF/Ndiaga Seck

Haiti: Huduma za kibinadamu na haki za binadamu zazidi kutwama

Kutoroka gerezani kwa zaidi ya wafungwa 4,500 nchini Haiti mwishoni mwa wiki iliyopita wakiwemo viongozi mashuhuri wa magenge ya uhalifu kukitajwa kuwa tishio la usalama wa taifa, huku huduma muhimu kama afya, elimu zikiendelea kuzorota kila uchao, Umoja wa Mataifa unataka hatua za haraka za jamii ya kimataifa kuzuia taifa hilo kuzidi kutumbukia kwenye ghasia.