Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Maelfu ya familia wamehama makazi yao kutokana na ukame wa hivi karibuni nchini Ethiopia
© UNHCR/Eugene Sibomana

Waziri wa mambo ya nje wa Uingereza atembelea waathirika wa ukame Ethiopia atoa ahadi ya kuendelea ushirikiano na UN

Waziri wa Mambo ya Nje wa Uingereza, James Cleverly akiambatana na Mwakilishi wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF Ethiopia, Gianfranco Rotigliano wametembelea eneo la Afar, nchini Ethiopia kujionea athari za ukame kwa watoto na familia na kutathimini hatua za dharura zizazochukuliwa na UNICEF ambapo Uingereza ni mdau muhimu kama mwanachama wa Umoja wa Mataifa na muhisani.

Sauti
2'12"
Mwanamke aliyezaliwa na VVU akipokea dawa kwenye kliniki nchini Burkina Faso
© UNICEF/Frank Dejongh

Ili kuumaliza UKIMWI lazima tuweke usawa duniani kote – Katibu Mkuu UN

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kupitia ujumbe wake wa Siku ya UKIMWI Duniani, siku ambayo huadhimishwa kila mwaka tarehe Mosi Desemba, amesema ili kuumaliza ugonjwa huo lazima kwanza kukomesha ukosefu wa usawa ambao unakwaza hatua za kusonga mbele katika mapambano dhidi ya ugonjwa huu unaohatarisha maisha ya watu ulimwenguni kote.