Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Ukosefu wa uwezo wa kifedha na kupata chanjo unakwamisha maendeleo ya uchumi wa nchi nyingi zinazoendelea
ILO/K.B. Mpofu

Asilimia 60 ya nchi za kipato cha chini Afrika ziko kwenye mzigo wa madeni:UNCTAD

Takriban asilimia 60 ya nchi za kipato cha chini barani Afrika hivi sasa ziko kwenye mzigo wa madeni, shinikizo kubwa au katika hatari ya kuingia kwenye madeni huku mamilioni ya Waafrika wakitumbukia tena kwenye umasikini wakati huu wakiwa kwenye hatari kubwa ya kutokuwa na uhakika wa chakula, imeonya ripoti mpya ya biashara na maendeleo kwa mwaka 2022 iliyotolewa leo na kamati ya Umoja wa Mataifa ya biashara na maendeleo UNCTAD.  

Sauti
2'54"
Choo kipya nyumbani kwa Agnes Djakwei kwenye mji mkuu wa Ghana, Accra, mradi huu ni wa Benki ya Dunia.
Video ya Benki ya Dunia

Huduma ya choo nyumbani yaleta nuru kwa kaya huko Accra ,Ghana

Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya makazi duniani, ujumbe ukiwa Zingatia pengo lililoko, usimwache  nyuma mtu yeyote au eneo lolote, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres anasema ukuaji wa miji lazima uende sambamba na uwekezaji siyo tu wa kuhakikisha kila mtu ana uwezo wa kupata nyumba ya  kuishi bali pia huduma muhimu kama vile za kujisafi, jambo ambalo huko nchini Ghana miradi inayowezeshwa na Benki ya Dunia imesaidia kaya ambazo zamani zilisubiri choo cha umma kisicho kisafi kujisaidia sasa zina huduma hiyo majumbani.

Sauti
2'25"
Wakimbizi kutoka Burundi wakichota maji katika kambi ya Lusenda, Kivu Kusini, Jamhuri ya Kidemkrasia ya Congo, DRC.
UNHCR/Colin Delfosse

Mlinda Amani wa Umoja wa Mataifa auwawa nchini DRC

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amelaani shambulio lililotokea hapo jana tarehe 30 Septemba 2022 nchini Jamhuri ya Kidemokrasia Kongo DRC katika kambi ya COB iliyopo chini ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO na kusababisha kifo cha mlinda amani mmoja raia wa Pakistan.