Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Ukatishaji wa huduma za kibinadamu unaathiri upatikanji wa maji Basse-Kotto Prefecture, CAR.
© UNOCHA/Virginie Bero

Ongezeko la mashambulizi dhidi ya wahudumu wa kibinadamu linatishia misaada kwa watu walio hatarini CAR - OCHA 

Mratibu wa Misaada ya Kibinadamu katika Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR, Bi. Denise Brown, kupitia taarifa iliyotolewa leo na Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu masuala ya kibinadamu na misaada ya dharura, OCHA, amelaani vikali ongezeko la mashambulizi dhidi ya mashirika ya kibinadamu, ambayo katika baadhi ya matukio yamelazimisha mashirika kusimamisha shughuli zao kwa ajili ya usalama wa wafanyakazi wao. 

UNICEF nchini Rwanda kwa kushirikiana na Bodi ya Madini nchini humo wamefanikiwa kuanzisha vituo viwili vya kulea watoto wadogo wenye umri kati ya miaka 0 mpaka 6 kwa ajili ya kusaidia wazazi wanaofanya kazi migodini.
UNICEF/2022/Mucyo

UNICEF Rwanda yawezesha uanzishwaji wa vituo vya kulelea watoto wa wafanyakazi wa migodi

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF nchini Rwanda kwa kushirikiana na Bodi ya Madini nchini humo wamefanikiwa kuanzisha vituo viwili vya kulea watoto wadogo wenye umri kati ya miaka 0 mpaka 6 kwa ajili ya kusaidia wazazi wanaofanya kazi migodini waweze kuwa na uhakika wa sehemu wanapowaacha watoto pindi waendapo kujitafutia kipato.

Sauti
3'10"