Ili kutimiza lengo la kutomwacha yeyote nyuma lazima tuwajumuishe watu wenye usonji:Guterres
Leo ni siku ya kimataifa ya uelimishaji kuhusu usonji na Umoja wa Mataifa unasisitiza haja ya kuwajumuisha watu wenye ulemavu ikiwemo wenye usonji ili kutimiza azma ya Malengo ya Maendeleo Endelevu SDGs ya kutomuacha yeyote nyuma.